Friday, May 17, 2013
LAANA: SERIKALI ICHUKUE HATUA KALI DHIDI YAO, PICHA ZA WANAFUNZI WA CHUO KIKONGWE CHA BIASHARA HAPA TZ WALIPONASWA WAKISAGANA.
![]() |
UNYAMA: POLISI AMCHARANGA MAPANGA MWANAE WA MIAKA 4 KISA KIKIWA NI WIVU WA MAPENZI

MTOTO WA MIAKA 4 DEVOTHA GERLAD ALIYEKATWA MAPANGA NA BABA YAKE,HAPA AKIWA HOSPITALI KWA HUDUMA AYA KWANZA.
WANANCHI WAKIWA NJE YA HOSPITALI YA WILAYA WAKIWA NA SHAUKU YA KUMUONA MTUHUMIWA.
KINA MAMA WALIOGUSWA NA TUKIO WAKIWA NJE YA HOSPITALI KUMUONA MTOTO HUYO.
HAPA AFANDE AKIWA HOI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALINI..
MADAKTARI WAKIJITAHIDI KUOKOA MAISHA YA MTOTO HUYO.
MUNGU AMPE AHUENI MTOTO HUYU.
chanzohttp://threewhite.blogspot.com
Wednesday, May 15, 2013
"MKITUKAZA KUNYWA VIROBA TUTAANZA KUNYWA GONGO"....WANANCHI WALIJIBU BUNGE
.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya
Viwanda na Biashara, wakiangalia uzalishaji walipotembelea kiwanda cha
Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Dar es Salaam hivi
karibuni.
Baadhi ya
wananchi jijini Dar es Salaam, wamelalamikia hoja iliyozuka bungeni wiki
hii kwamba kinywaji cha Konyagi aina ya Kiroba kipigwe marufuku nchini.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao, walisema endapo serikali itachukua uamuzi wa kupiga marufuku kinywaji hicho,watarudia kunywa pombe aina ya gongo ambayo ni hatari kwa afya zao.
Mkazi wa Mbagala, Faustine Mwiruka aliyekutwa kwenye baa ya Kisuma, aliiasa Serikali kutothubutu kukubali kinywaji hicho kupigwa marufuku, kwani ikifanya hivyo wengi wa wananchi wenye kipato cha chini wataanza tena kunywa gongo na pombe za kienyeji.
Itabidi tufanye kama Zambia ambao wamezuia viroba, lakini nchi nzima imejaa viroba vya Malawi, Zaire na Burundi, lazima tuiadhibu serikali ikose kodi kote kote, bia hatunywi, viroba vya nje tutakunywa, pamoja na gongo.
Alisema haingii akilini kukihusisha kinywaji hicho na ajali za magari, akidai kuwa hata kabla ya viroba kuingia sokoni ajali zilikuwepo nyingi.
“Sisi tuna imani na viroba kwa vile vina ubora wa uhakika tofauti na pombe ya gongo ambayo inapikwa bila kupimwa ubora hivyo ni hatari kwa usalama wa afya zetu.” amesema Mwiruka.
Naye Ali Hassan mkazi wa Kinondoni kwa Manyanya, alisema, wanaotaka viroba vipigwe marufuku hawawatendei haki wananchi wa kawaida ambao kwa asilimia kubwa hawana uwezo wa kununua bia ambazo bei yake ni kubwa.
Mwandishi wetu aliyetembelea maeneo ya Ilala Kota Mchikichini alifanikiwakuhojiana na wakazi wa eneo hilo ambao wengi wao walisema kuwa jambo hilo lililozushwa wiki iliyopita wanaamini ni njama za wafanya biashara toka nchi jirani ambao hawaitakii mema Tanzania kwa kuwa pombe hiyo kuwepo kwake pia kunakuza pato la Taifa.
Juma Pingu amesema kuwa haoni sababu ya kupiga marufuku viroba kwakuwa ni pombe ya wanyonge na kuwataka wabunge kuthamini bidhaa za nyumbani kwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari mwanzoni mwa wiki hii, Mkurungenzi Mkuu wa Konyagi, David Mgwassa amesema kuwa kwa kipindi kirefu kumekuwa na mchezo mchafu wa kuharibiana jina sokoni kwa kutumia baadhi ya vyombo vya habari vya hapa nchini, kampeni inayoendeshwa na makampuni yenye uhusiano na makampuni makubwa ya pombe duniani yasiyo penda, nchi za afrika zizalishe pombe zake, bali ziendeleee kununua kutoka Ireland, wales. Kenya and uingereza.
Wadau hao wa Pombe nchini walifikia uamuzi wa kutoa maoni hayo baada ya kuona kuwa kinywaji chao Kiroba kinapigwa vita lukuki kwenye magazeti. Huwezi ukahusisha viroba na piki piki, kwani nchi hii ina piki piki laki tatu, na wananchi million 43, uhusiano wake uko wapi, kwanza hata leseni hamuwapi?
‘Mapepo’ yasababisha shule kufungwa

Kamanda wa Polisi Kinondoni, Charles Kenyela
Dar es Salaam. Wanafunzi wa Sekondari ya Kata ya
Manzese, wamedai kutokewa na hali isiyoeleweka na kusababisha wenzao 32
kuanguka na kupoteza fahamu kwa nyakati tofauti.
Tukio hilo lilianza saa 2:35 asubuhi na kudumu
hadi saa 6:00 mchana. Kutokana na hali hiyo, uongozi wa shule hiyo
umesitisha masomo kutwa nzima ya jana ili kuwahudumia wanafunzi hao na
kuwaruhusu wengine kurudi nyumbani hadi kesho.
Mkuu wa sekondari hiyo alipofuatwa ofisini kwake
kuzungumzia suala hilo, alikutwa akiombewa na Mchungaji wa Kanisa la
Tanzania Assemblies of God (TAG), ambaye baadaye alijitambulisha kwa
jina la Godfrey Alphonce maarufu kama Punda wa Yesu.
Mchungaji huyo baada ya kumaliza ibada hiyo, Mkuu
wa shule alitoka akiwa ameambatana na watu wengine na alikataa
kuzungumza na waandishi wa habari waliokuwapo.
“Nimechanganyikiwa naomba uniache, akili yangu haipo vizuri,” alisema mwalimu huyo na kupanda gari kisha kuondoka eneo hilo.
Kamanda wa Polisi Kinondoni, Charles Kenyela alipulizwa kuhusiana tukio hilo, alisema ofisi yake haijapata taarifa.
CHANZO MWANANCHI
HIKI NDO KIASI ALICHOINGIZA MWANA FA KWA KUUZA RBT, KWELI HIP HOP INAUZA

Akiongea leo kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, FA aliyekuwa wa tatu kati ya wasanii waliopata fedha nyingi zaidi kwenye malipo hayo chini ya Rose Mhando na Diamond, amesema ameamua kuweka wazi hilo ili watu waondoe imani kuwa muziki wa hip hop hauuzi.
Tarehe 31 mwezi huu, Mwana FA ambaye jina lake halisi ni Hamis Mwinjuma atakuwa na show yake aliyoipa jina, The Finest.
chanzobongoclantblog
Saturday, May 11, 2013
MAZISHI YA WALIOUAWA KWA MABOMU WAZIKWA,MAJONZI YATAWALA,MAASKOFU WATOA KILIO CHAO KWA WAZIRI MKUU
![]() |
Majeneza yakiwa kanisani kabla ya ibada ya mazishi
|
![]() |
Mapadri wakiwa wamebeba moja ya majeneza |
![]() |
Watawa wakiwa kanisani wakati wa ibada |
![]() |
Viongozi wa Kanisa wakitoa salamu za mwisho |
![]() |
Kilio kilio kilio anamlilia mama yake mzazi |
![]() |
Wananchi wakitoa salamu zao za mwisho kwenye kanisa katoliki |
![]() |
Majonzi na uchungu |
![]() |
Wahudumu wakishusha mwili wa marehemu kaburini kwenye viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olasiti jijini Arusha |
![]() |
Wahudumu
wakishusha mwili wa marehemu kaburini kwenye viwanja vya Kanisa la
Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olasiti jijini Arusha |
![]() |
Baadhi ya maaskofu kutoka majimbo mbalimbali waliohudhuria ibada ya mazishi leo |
![]() |
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania(KKKT)Dk Alex Malasusa(kushoto)akiwa na viongozi wengine wa Kanis a hilo wakiwa kwenye ibada ya mazishi |
![]() |
Umati wa watu waliohudhuria maziko hayo |
![]() |
Waziri Mkuu mstaafu,Edward Lowassa(kulia)akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani,Dk Emmanuel Nchimbi kabla ya ibada kuan |
RAIS JAKAYA KIKWETE AREJEA NCHINI TOKA AFRIKA KUSINI LEO
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib
Bilali (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Raymon Moshi mara baada ya
kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar
es salaam leo Mei 11, 2013 akitokea Cape Town, Afrika ya Kusini,
alikohudhuria mkutano wa nchi SADC
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib
Bilali (kulia) mara baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Mei 11, 2013 akitokea Cape
Town, Afrika ya Kusini, alikohudhuria mkutano wa nchi SADC.PICHA NA
IKULU
Subscribe to:
Posts (Atom)