BUNGE MAALUM LA KATIBA LAAHIRISHWA KUTOKANA NA VURUGU.

Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba Mh. Pandu Kificho ameahirisha
Semina ya kujadili Kanuni za Bunge Maalum la Katika Kutokana na
Vuruguru na Hali ya Kutokuelewana Kati ya Mbunge wa Jimbo la Simanjiro
Mh Ole Sendeka Kutoleana maneno na Mbunge Mwenzake wakati Mbunge Huyo
alipohoji kuhusu Kanuni hizo.
Bunge
Maalumu la Katiba linalokutana mjini Dodoma leo limeingia dosari
kufuatia vurugu kubwa zilizotokea ndani ya ukumbi wakati wajumbe
wakichangia maoni katika kifungu cha 58 cha kanuni za uendeshaji, hali
iliyosababisha kuahirishwa kwa muda.
Chanzo
cha vurugu hizo kilianzia kwa Waziri wa Sheria na Katiba wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Abubakari Hamisi Bakari alipomweleza mwenyekiti
kuwa jina la Christopher Ole Sendeka halikuwa katika orodha ya majina ya
wachangiaji.
Bakari amesema kitendo kama hicho ambacho kilimfanya mjumbe mwingine Ummi Mwalimu kuzuiwa kuchangia kingeweza kulifanya Bunge likaendelea kujadili kanuni hadi miezi sita kwani tabia ya kuruhusu majina inafanywa na Sekretarieti kinyemela.
Bakari amesema kitendo kama hicho ambacho kilimfanya mjumbe mwingine Ummi Mwalimu kuzuiwa kuchangia kingeweza kulifanya Bunge likaendelea kujadili kanuni hadi miezi sita kwani tabia ya kuruhusu majina inafanywa na Sekretarieti kinyemela.
Hali
hiyo imemkera Ole Sendeka na kulazimika kutoa maneno ya kejeli kwa
Bakari akieleza kwamba anazijua sheria kuliko waziri huyo huku
akimtuhumu kuwa ana ajenda yake ya siri katika kukwamisha mchakato huo.
Kauli
ya Ole Sendeka illipua hisia za wengi na karibu nusu ya wajumbe
walisimama na kuanza kupigizana kelele wakimtaka aombe radhi hatu ambayo
iliungwa mkono na mwenyekiti wa muda wa bunge hilo Pandu Ameir Kificho.
Hata
hivyo, hali ilikuwa mbaya zaidi pale alipopewa nafasi bakari ambaye
alikejeli kuwa anazijua sheria vizuri kwani tangu mwaka 1980 amekuwa
katika mabunge hayo kuliko Ole Sendeka ambaye ametokea Simanjiro miaka
10 iliyopita.
Kufuatia mvutano huo utulivu wa Bunge ulipotea, kwani kila upande ulianza kupiga kelele na kuwasha vipaza sauti hali iliyosababisha Kificho kuahirisha shughuli za bunge hilo hadi saa 10 hii jioni.
No comments:
Post a Comment