Sehemu ya waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano na Katibu Mkuu wa EAC,Dk Richard Sezibera leo
Katibu
Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,Balozi Dk Richard Sezibera amesema
mgogoro kati ya Rais wa Tanzania,Dk Jakaya Mrisho Kikwete na mwenzake wa
Rwanda,Paul Kagame hauwezi kuathiri kwa kiwango cha kuvunja jumuiya
hiyo japo sio afya kwa juhudi za mtangamano.
Amesema jitihada za
kuutatua mgogoro zinafanywa na EAC pasipo kutaka kuingiliwa na vyombo
vya habari na kua njia pekee ya kuumaliza ni kwanjia ya kidiplomasia.
"Tunaendelea
na mashauriano ambayo hatujapenda vyombo vya habari kuingilia kwa
sasa,tunaamini njia sahihi ni njia ya kidiplomasia zaidi"
Hata
hivyo alikanusha taarifa zilizoenea kuwa wafanyakazi wa Tanzania na
Rwanda wanaofanya kazi EAC wamekuwa hawasemeshani kutokana na mgogoro
huo.
Dr Sezibera akizungumzia raia wa kigeni walioamriwa kuondoka
mkoani Kagera ,alisema anaamini kila nchi ina utaratibu wake lakini
hakuna sababu ya kuwaita raia wa Afrika Mashariki wahamiaji haramu
kwani wananchi wa eneo hili ni wamoja.
Alisema Kanda ya Afrika
Mashariki inakabiliwa na migogoro mikubwa ukilinganisha na maeneo
mengine yakiwamo makundi yaliyofanya mauji ya kimbali na mengine kama
kikundi cha FNL cha Burundi na mengine jambo linalohatarisha usalama kwa
ujumla.
|
No comments:
Post a Comment