ZITTO NA DEMOKRASIA
Zitto na Demokrasia
PRESS RELEASE: ZITTO ZIARANI ULAYA
PRESS RELEASE
Zitto aenda Uswiss na Uingereza kuhusu utoroshaji wa fedha
Shirika la Kimataifa la Mtandao wa Ulaya wa Madeni na Maendeleo, European Network on Debt and Development (Eurodad) watafanya
ziara ya kiuchunguzi kuhusu masuala ya uwazi katika kodi katika nchi za
Ulaya kuanzia tarehe 20 Oktoba mpaka tarehe 5 Novemba mwaka 2013.
Uchunguzi huo utaendeshwa na wataalamu waliobobea wa masuala ya kodi na
maendeleo. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali wa Bunge
la Tanzania Zitto Zuberi Kabwe ameteuliwa kuongoza Jopo la uchunguzi
huo.
Eurodad ni Mtandao wa Mashirika yasiyo ya kiserikali yapatayo 48 kutoka
nchi 19 za Ulaya ambayo yanajihusisha na masuala ya kufutia madeni nchi
zilizoendelea, misaada yenye maana na kodi za haki. Mashirika haya
yamekuwa kwenye kampeni ya kupinga utoroshwaji wa fedha kupitia ukwepaji
kodi unaofanywa na mashirika ya kimataifa kwa nchi zinazoendelea. Zitto
amekuwa mmoja wa wabunge wanaosimamia hoja ya kutaka Watanzania
waliotorosha fedha kwenda nje warejeshe na kufunguliwa mashtaka. Mwaka
2012 aliwasilisha hoja binafsi Bungeni na kupitishwa kuwa Azimio la
Bunge ya kutaka uchunguzi kuhusu utoroshwaji wa fedha na kufichwa nje
kama Uswiss. Kikosi Kazi cha Serikali kutekeleza Azimio hilo la Bunge
kinatarajia kuwasilisha taarifa yake katika Mkutano wa Kumi na Sita wa
Bunge. Siku ya Jumatatu tarehe 21 Oktoba Zitto atakutana na Waziri wa
Fedha wa Uswiss na maafisa wa mabenki na asasi zisizo za kiserikali
zilizopo jijini Geneva. Pia Zitto atahudhuria mkutano wa Kamati ya Kodi
ya Umoja wa Mataifa katika kampeni ya kubadili mfumo wa kodi za
kimataifa ili kuzuia unyonyaji wa nchi za Kiafrika unaofanywa na
Makampuni makubwa ya Kimataifa.
Baada ya Geneva Zitto atatembelea nchi za Luxembourg na Brussels kabla
ya kwenda Norway ambapo atamalizia ziara yake kwa Jopo la Wataalamu wa
masuala ya kodi na Maendeleo kuandika taarifa maalumu yenye mapendekezo
kuhusu kuzuia utoroshaji wa fedha kutoka Afrika.
Zitto atakwenda jijini London kutoa mada kuhusu masuala ya kodi za
kimataifa katika mkutano wa Uwazi (Open Government Partnership).
Mwenyekiti wa PAC Tanzania atafanya mazungumzo na Mwenyekiti wa PAC
Uingereza Bi Margaret Eve Hodge, Lady Hodge MBE, PC, MP kuhusu masuala
mbalimbali ya ushirikiano wa mabunge mawili na kuendeleza wito wake kwa
makampuni ya kimataifa kulipa kodi zao barani Afrika na kuacha tabia ya
kutumia ‘Tax Havens’ kukwepa kodi na kufukarisha nchi za Kiafrika.
Zitto invited to annual OGP Summit
The Kigoma North Member of Parliament and Chairman of the Public
Accounts Committee (PAC), Hon Zitto Kabwe has been invited for the
annual Open Government Partnership (OGP) Forum which kicks off in London
at the end of the month.
The OGP Summit is a chance to promote tax and illicit issues to new
audiences, to encourage new commitments in country action plans.
Hon Zitto, who also serves as Deputy Leader of Official Opposition in
the Parliament, will serve in the panel which will discuss tax and
illicit flows, which is among themes to be deliberated during the
summit.
The OGP is a global platform for domestic reformers committed to making
their governments more open, accountable, and responsive to citizens.
Tanzania is among countries which have signed its membership to the OGP.
Hon Zitto has great interest on tax avoidance through illicit transfers
and last year he tabled private motions which lead to the adoption of a
Parliament Resolution compelling the government to investigate a number
of individuals who have illicitly stashed billions of dollars abroad.
The fact finding mission will see its members interact with UN Tax
Committee, OECD, EU as well as key European governments. They will visit
a number of European cities namely Geneva, Paris, Luxembourg, Brussels
and Oslo.
No comments:
Post a Comment