Wednesday, April 23, 2014

TAASISI MBALIMBALI ZA KILIMO JIJINI ARUSHA ZINATARAJIA KUKUTANA NA WAKULIMA ZAIDI YA 500 KWA AJILI YAMAONYESHO YA KILIMO KANDA YA KASKAZIN
 Mkurugenzi wa Tanzania Horticulture Association(TAHA) bi,Jackline Mkindi akizungumza na vyombo vya habari ambao hawapo pichani juu ya maonesho ya kilimo ambao yanatarijiwa kufanyika siku ya Aprili 25 na 26 katika viwanja vya AVRDC vilivyopo eneo la Tengeru wilayani arumeru mkoani arushakilia kwake ni Mratibu wa Agri-Hub Tanzania bw,Tom ole sika


afisa mtendaji mkuu wa Taha (wa pili kulia)  Akitoa taarifa kwa waandish wa habri

Taasisi mbalimbali za kifedha pamoja na mashirika mbalimbali wanatarajiwa kukutanishwa na taasisi za kifedha 48 ili kuweza kuongeza ufahamu na uelewa juu ya huduma mbalimbali za nkifedha zitolewazo na mabenki,taasisi ndogo ndogo za kifedha,mashirika ya bima,taasisi za elimu na mashirika yasiyo ya kiserikali.


Ameyasema hayo wakati akizungumza na vyombo vya habari   bi.Jackline Mkindi na kusemakuwa wakulima wadogo wadogo wamekukwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya ya upatikanaji wa huduma za kifedha hususani kwa wadau wa sekta ya kilimo.


Katika kutatua changamoto hiyo ya mitaji Agri-Hub Tanzania ikishirikiana na TAHA mashirika,asasi  mbalimbali kwa umoja wao wamethamiria kuwaunganisha wadau wa kilimobiashara na watoa huduma za kifedha moja kwa moja ili pande zote mbili ziweze kukuelewana na juu mahitaji yao na hatimaye watoa huduma za kifedha waweze kubuni huduma bora zaidi za kuimarisha utoaji huduma zao kwa wadau wa kilimo.


Mkindi alisem kuwa maonesho hayo yatakwenda sambamba na uwasilishwaji wawa mada mbalimbali ikiwemo uaandaaji bora wa wa mpango biashara (business plans),umuhimu wa wa soko la hisa katika kuhakikisha upatikanaji wa mitaji  ya muda mrefu na matumizi bora ya mikopo katika biashara hususani za kilimo.


Hata hivyo mtaribu kutoka kampuni ya Agri-Hub Tanzania bw,Tom Ole Sikar,alisisitiza kuwa maonesho hayo yanalenga kuwawezesha wakulima wajasiriamali pamoja na wamiliki wa biashara za kilimo kama wachuuzi,wauzaji wa pembejeo na wasindikaji kutambua fursa mbalimbali za mitaji na usalama wa kifedha(Financial security) zilizopo kwa biashara za kilimo.


  Pamoja na hayo sikar alisema kuwa wadau hao wataweza kuunganishwa na taasisi muhimu za  fedha ikiwa ni pamoja na kushiriki katika mawasilisho na majadilino juu ya fursa za sekta binafsi katika kilimo pamoja na wataalamu wa mambo ya fedha na watoa huduma za maendeleo ya biashara kupitia semina zitakazotolewa sambamba na maonesho hayo.


‘’maonesho hayo yatawawezesha wadau kutambua njia za kuboresha biashara na utoaji wa huduma kwa walengwa ikiwa ni pamoja na kujifunza kutoka kwa wafanyabiashra wengine wa kilimo waliofanikiwa kutembelea maonesho “alisema bw,Sakar


Maonesho hayo yanatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Taasisi ya AVRDC(The World Vegetable Centre) kuanzia tarehe 25  na 26 april kuanzia majira ya saa tatu aubuhi mpaka saa kumi na moja jioni.
  Hata hivyo katika maonyesho hayo wakulima pamoja na wadau mbalimbali wa kilimo wanatarajiwa kuhudhuriwa na kiingilio itakuwa ni bure kabisa



 
cid:image912EFE08-5FD1-4D97-B049-B6F5BE57643A



BY.GODFREY THOMAS

No comments:

Post a Comment